February 20, 2013




Baada ya kupoteza mchezo wa jana wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuchapwa mabao 3-1 na Bayern Munich, hakuna ujanja na nafasi ni ndogo kwa Arsenal kusonga.
Iwapo itashindwa kusonga, kinachoonekana sasa katika timu hiyo kinatakiwa ni makombe na si kingine. Kwani kama fedha wanazo.
Kweli kama watafikia uamuzi wa kubadili kocha msimu ujao, chaguo sahihi la Arsenal litakuwa ni Jose Mourinho ingawa kuna mambo mengi watalazimika kuyabadili.
Kwanza ni klabu kutokuwa tayari kutoa mamilioni kununua wachezaji, kitu kizuri ni kwamba Mourinho si mtumiaji wa mafedha sana, lakini ni tofauti na Wenger.
Tokea mwaka 2003 alipotwaa ubingwa wa Ureno akiwa na FC Porto, kila mwaka amekuwa akichukua kikombe katika kila ligi aliyokuwa anafundisha timu fulani.
Mourinho aliahidi ubingwa tokea siku ya kwanza alipotua Chelsea, kweli alifanya hivyo ikiwa ni pamoja na kuchukua ubingwa wa Kombe la FA, pia wakafika fainali ya ligi ya mabingwa na kushindwa kwa penalti na Man United jijini Moscow.
Kama wanataka kuendelea kubana matumizi, Arsenal hawana ujanja wanaweza kuendelea kubaki na Wenger, kama ni vikombe, hakuna ujanja, Mourinho ambaye mambo yake hayaendi vizuri Madrid, ndiye chagu sahihi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic