February 20, 2013





Baada ya kuhaha kwa zaidi ya wiki moja na nusu akitaka kulipwa fedha zake dola 32,000 kutoka kwa uongozi wa Simba, hatimaye ‘zali’ limemuangukia.
Milovan raia wa Serbia, ameahidiwa kulipwa fedha zake na makamu mwenyekiti wa kamati ya fedha, Rahma Al Kharusi maarufu kama Malkia wa Nyuki.
Mwanamama huyo jana alikata mzizi wa fitina na kupitisha kumlipa Milovan kwa fedha zake huku akisema ameamua kuiondolea Simba aibu.
“Simba ina mambo mengi, lakini sasa hakuna kinachoendelea. Leo wanachama wanachanganyikiwa, hawajui wapi pa kushika. Mambo hayaendi vizuri kwenye klabu, huku kocha huyu anadai.

“Sasa anzunguka tu mitaani anasema maneno, kweli anadai haki yake, kwa nini tusimpe. Mimi sipendi ubabaishaji, nitamlipa,” alisema Rahma.
Baada ya mazungumzo ya takribani dakika nne na Rahma aliomba namba za akaunti ya Milovan na kuahidi kumtumia fedha zake ndani ya siku tatu.
Rahma ambaye aliondoka jana nchini kwenda Oman, alisema atatuma fedha hizo kwa Milovana na kumtaka awe na subira hadi atakapotua Oman leo usiku.

Milovan ambaye alikuwa kama ameshangazwa na hali hiyo kwa kuwa kesho alipanga kutua TFF kufikisha mashitaka yake, alisema amefurahishwa sana na Malkia wa Nyuki.
 Pamoja na kumlipa, Malkia wa Nyuki aliutaka uongozi wa Simba kufanya mambo kwa uwazi na usahihi.

“Sidhani kama ni sahihi watu wanafanya mambo kwa kulipua tu, nafikiri huu ndiyo wakati mzuri wa wao kuamua kushughulika na timu au kwenda kwenye siasa.
“Mwendo wa Simba si mzuri, huyu kocha hauwezo kujua inawezekana kesho tukamhitaji tena, tunachofanya hiki si sahihi.
“Nataka niwaambie kitu, mimi si mtu wa kubabaishwa, simhofii mtu yoyote na ninafanya mambo yangu kwa mpangilio. Hiyvo nataka kufanya kazi na watu walio makini,” alisema.
Milovan aliyeanza kwa mara ya kwanza kuifundisha Simba mwaka 2008, alikuwa amepanga kutua TFF kesho kufungua mashitaka yake.
Viongozi wa Simba, Jumapili iliyopita walikimbia uwanjani mara baada ya timu yao kupata kipigo cha bao moja kutoka kwa wageni wao Recreativo Libolo ya Angola.
Hali hiyo imezua mjadala mkubwa, kwamba kwa nini kama viongozi walikimbia wakati jahazi linazama? Lakini timu inaposhinda wanabaki na kusherekea ushindi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic