Kocha
Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts ametuma salamu kwa wapinzani wao Azam FC kwamba
mechi ya Jumamosi watakuwa katika wakati mgumu.
Brandts
ambaye kikosi chake kimejichimbia mjini Bagamoyo kujiandaa na mechi gumzo ya
Ligi Kuu Bara, amesema ana imani mchezo huo utakuwa mzuri na wa kuvutia, lakini
wao wanachotaka ni pointi tatu.
“Sina
hofu na kikosi changu, tumekuwa tukiendelea na mazoezi vizuri. Kama binadamu
kuna mambo kadhaa yanaweza kutufanya tusifikie tunachotaka, lakini pointi tatu
bado ni muhimu sana kwetu.
“Bado
tunaiheshimu Azam FC kama moja ya timu bora kabisa, lakini nimewaambia vijana
wangu kikosi chetu ni bora zaidi na ushindi ni muhimu hasa Jumamosi.
“Ushindi
wa Jumamosi ni hesabu bora kabisa kwetu, kikosi kinaturuhusu kufanya vizuri.
Lakini nimesisitiza umakini na kutumia nafasi tutakazozipata ili baadaye
tusijalaumu,” alisema Brandts raia wa Uholanzi.
Mchezo
huo umekuwa gumzo kubwa miongoni mwa wapenda soka, kila upande ukiamini
ukishinda ndiyo safari ya kuufuata ubingwa.
Kila
timu ina pointi 36 ingawa Azam FC wana mchezo mmoja zaidi, wakati Yanga ina
mchezo mkononi lakini Brandts amesisitiza ushindi lazima.
0 COMMENTS:
Post a Comment