MLEZI wa Simba, Rahma Al Kharusi amefanya kufuru baada
ya kumlipa kocha wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic fedha zaidi ya alizokuwa
anadai.
Rahma maarufu kama Malkia wa Nyuki amemlipa Milovan
dola 35,000 (Sh milioni 56) wakati alikuwa anadai dola 32,000 (Sh milioni 51.2).
Akizungumza jana kutoka Muscat, Oman, Malkia wa Nyuki
alisema ameamua kulipa dola 3,000 (Sh milioni 4.8) zaidi ili kocha huyo aweze
kulipa deni la hoteli anayokaa.
“Nilihofia wasije wakamsumbua kuhusiana na kulipa hoteli,
kama watamlipia basi hiyo dola 3,000 yeye anaweza kutumia katika mambo yake
mengine,” alisema.
“Nataka akiondoka aende kwa amani, hakuna haja ya
kugombana na watu, kwa mujibu wa taratibu za benki, ikifika Jumatatu yeye aende
tu akaangalie akaunti yake.”
FOMU YA MALIPO...
Malkia wa Nyuki aliahidi juzi kumlipa Milovan deni
hilo baada ya uongozi wa Simba kuwa umemzungusha huku viongozi wake wakuu
wakimkimbia kocha huyo aliyekuwa anadai mshahara wa miezi mitatu kwa ajili ya
kuvunja mkataba na mwezi mmoja aliokuwa anadai.
0 COMMENTS:
Post a Comment