Mshambuliaji
wa zamani wa Simba, Emmanuel Okwi sasa amehamishiwa katika kitengo cha kuongeza
nguvu na ameanza mazoezi ya gym.
Benchi
la ufundi la timu yake ya Etoile du Sahel ya Tunisia, limempeleka Okwi na
baadhi ya wachezaji katika gym ya timu hiyo.
Pamoja
na mazoezi ya gym, Okwi amekuwa akiendelea kufanya mazoezi na wenzake kwa
kucheza nao mpira ingawa bado hajaanza kucheza mechi za timu hiyo.
Hivi
karibuni, Okwi ambaye alikuwa tegemeo la ushambuliaji katika kikosi cha
mabingwa wa Tanzania Bara, Simba alisema ataendelea na programu ya mazoezini
pembeni kabla ya kuanza kucheza.
Tokea
ametua nchini humo, Okwi hajaanza kuichezea timu hiyo zaidi ya kuendelea na
mazoezi. Kawaida amekuwa akicheza mechi za mazoezini ambazo zinahusisha
wachezaji wa timu hiyo.
Haina
shaka, Mganda huyo akianza kucheza ataonyesha makali aliyonayo ambayo
yaliushawishi uongozi wa Etoile du Sahel kutoa kitita cha dola 400,000
kumsajili.
Okwi
ambaye analamba mshahara wa dola 15,000 kwa mwezi alilipwa dola 100,000 kwa
ajili ya usajili, huku Simba ikipata dola 300,000 ingawa kumekuwa na taarifa
Msimbazi walikamata ‘mahela’ zaidi.
0 COMMENTS:
Post a Comment