Baada ya kuamka na ushindi wa bao 1-0
dhidi ya wenyeji wao Prisons ya Mbeya jana, mabingwa wa soka Tanzania, Simba
wameamua kupasha ‘msuri’ kwa kubaki mjini humo.
Leo jioni, Simba itacheza mechi ya
kirafiki dhidi ya kikosi cha Mbeya City ambacho kimepanda daraja hadi Ligi Kuu
Bara msimu ujao.
Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri
Kihwelo amethibitisha Simba kubaki Mbeya na kucheza mechi ya kirafiki.
“Tumeamua kufanya mazoezi kidogo,
baada ya hapo tutaondoka kurudi Dar. Tunajua hii ni sehemu ya mazoezi nab ado kuna
makosa tunaendelea kurekebisha,” alisema Julio.
Pamoja na kufanikiwa kupata sare ya
bao 1-1 dhidi ya wenyeji wake Galatasaray jana usiku, Schalke 04 wametishia
kumkatia rufaa mshambuliaji Didier Drogba.
Schalke 04 wametangaza kukata rufaa
Uefa kuhusiana na Galatasaray kumtumia Drogba katika mechi za Ligi ya Mabingwa
Ulaya.
Hata hivyo, Schalke 04 wameonekana
kuficha ‘silaha’ wanayoitumia baada ya kushindwa kuweka wazi tatizo ni lipi.
Drogba anaonekana kutokuwa na tatizo
la kuichezea timu hiyo kwani tokea aipe ubingwa Chelsea, hajawahi kucheza
michuano hiyo na aliondoka kwenda kujiunga Shanghai Shenhua ya China.
Hata hivyo kuna taarifa, Schalke
wanaweza kutumia kipengele cha Shanghai Shenhua kusisitiza bado ina mkataba na
Drogba.
Drogba aliichezea Galatasaray mechi
yake ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa dhidi ya Schalke na matokeo
yalikuwa sare ya 1-1. Anategemea kuiongoza klabu yake hiyo mpya katika mechi ya
marudiano.
0 COMMENTS:
Post a Comment