Wababe wa
Uturuki wakiwa nyumbani, usiku wa kuamkia leo Alhamisi walishindwa kuonyesha
cheche zao baada ya kulazimishwa sare.
Galatasaray
walikuwa nyumbani Istambul kuwakaribisha Wajerumani, Schalke 04 katika mechi ya
Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya 16 Bora iliyomalizika kwa sare ya bao 1-1.
Kwa mara
ya kwanza, Didier Drogba aliichezea timu yake hiyo mpya katika mechi ya Ligi ya
Mabingwa Ulaya lakini hakufanikiwa kufunga.
Wenyeji
walipata bao la mapema kupitia kwa Burak Yilmaz lakini Jermaine Jones
akasawazisha ‘usiku’ na kuwafanya Galatasaray kuwa na kibarua kigumu katika
mechi ya marudiano nchini Ujerumani.
Kama
ilivyo kawaida yao, mashabiki walijitokeza kwa wingi Turk Telekom Arena
kuishangilia timu yao lakini Wajerumani hao ambao wanaonekana kuwa tishio
katika michuano hiyo walionekana kuwa wabishi zaidi.
0 COMMENTS:
Post a Comment