February 20, 2013


INGAWA kila upande umeonyesha kuwa suala kukutana kwao ni kama sehemu ya mazungumzo, lakini tayari kuna fununu huenda Yanga ikamvuta kocha wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic.

Uongozi wa Yanga unaamini Milovan anayehaha kuidai Simba fedha zake ni mmoja wa makocha bora kabisa hasa katika ngazi ya kukuza wachezaji vijana wanaochipukia katika soka.

Wakati akiwa Simba, alionyesha kwamba analiweza hilo baada ya kutoa nafasi kwa vijana wengi waliokuwa hawapewi nafasi kama vile Shomari Kapombe, Jonas Mkude, Haruna Chanongo, Abdallah Seseme na Ramadhani Singano ‘Messi’.

 

Milovan alitoa nafasi kwa vijana zaidi ya hao na kuwapa majukumu makubwa na mwisho wakaaminika hadi katika kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars, kitu ambacho kilimjengea zaidi jina lake.

Taarifa zinaeleza suala hilo liko katika mjadala, Ernie Brandts ataendelea kuwa kocha wa timu kubwa na Milovan akuze vijana ambao atamkabidhi Mholanzi huyo.

Hata hivyo, suala hilo linafanywa kwa umakini mkubwa na viongozi wa Yanga wamekuwa wagumu kulizungumzia hadharani huku ikionekana kuwa kuna jambo linafuatia.

Hata hivyo picha zilizonaswa wakiwa Milovan na viongozi wa sasa na wale wa zamani wa Yanga ni dalili ya kuonyesha kuna jambo.

Milovan mwenye amesisitiza ni mazungumzo ya kawaida tu, kama alivyozungumza na gazeti la michezo la CHAMPIONI ambalo leo limetoka na picha zake akiwa na viongozi hao wa Yanga.

Salehjembe inaendelea kufanya uchunguzi wa jambo hilo ikiwa ni pamoja na kufuatilia lini Milovan atalipwa na Simba kwa kuwa viongozi wake wameshasambaratika.

 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic