Kipa
namba moja wa Simba na timu ya taifa, Juma Kaseja ameungana na wachezaji nyota
wa duniani kwa viatu vyake kuandikwa jina.
Wachezaji
wengi nyota kama Lionel Messi, Ronaldo, Wayne Rooney na wengine kibao viatu
vyao vimekuwa na majina yao kama ilivyo katika jezi.
Ingawa
si kitu cha kawaida kwa wachezaji wa Tanzania kuonekana viatu vyao vikiwa na
majina yao.
Kaseja
alionekana akiwa na kiatu aina ya Nike chenye jina lake wakati Simba ilipoivaa
Libolo ya Angola na kulala kwa bao 1-0.
Hii
si mara ya kwanza mchezaji huyo maarufu zaidi katika kipindi cha miaka mitano
nchini kujumuika na wachezaji maarufu.
Hata
hivyo haijajulikana mara moja kama Kaseja kapata ‘shavu’ la udhamini wa Nike,
au aliamua kufanya utundu mwenyewe na kuandika jina lake.
Hivi
karibuni alipata tenda ya kutengeneza tangazo la Pepsi ambalo alijumuishwa
katika picha moja na nyota kama Messi, Thierry Henry, Fabregas na wengine
kibao.
0 COMMENTS:
Post a Comment