Nyota wa
Real Madrid, Cristiano Ronaldo alikuwa rubani wa ndege kwa muda, taarifa ambazo
zimezua gumzo.
Imeelezwa
Ronaldo mwenye miaka 28, alipata nafasi ya kuiendesha ndege ikiwa angani kwa
dakika chache tu. Hata
hivyo haijajulikana Ronaldo aliendesha ndege ipi na wapi, hali ambayo imezua
maswali mengi.
Taarifa
zinaeleza, huenda jambo hilo linafanywa siri kwa marubani waliompa ruhusa hiyo
kuonyesha kuhofia adhabu ya kukiuka maadili ya taaluma yao.
Pamoja na
marubani hao kuficha, Ronaldo ndiye anaonekana kutibua mambo baada ya kuweka
picha katika mtandao wa kijamii wa Twitter akiwa anaendesha ndege hiyo.
Waliotoa
maoni, wengi walimtaka kuelekeza mawazo yake katika mechi ya marudiano dhidi ya
Man United na si ‘mambo ya kitoto’.
0 COMMENTS:
Post a Comment