February 25, 2013




Swansea City imefanikiwa kuchukua ubingwa wa Kombe la Capital One kwa kishindo baada ya kuifunga Bradford kwa mabao 5-0 na kuweka rekodi.

Timu hiyo inayosifika kwa kutandaza soka la chini ilifanikiwa kutwaa ubingwa, hivyo kuwa timu ya tatu kwa ushindi wa mabao mengi katika fainali tokea Bury ilipoifunga Derby County 6-0 katika fainali ya mwaka 1903. Nafasi ya pili ya ushindi mkubwa iko kwa Blackburn Rovers iliyoshinda 6-1 dhidi ya The Wednesday mwaka 1890.

Katika mechi hiyo kwenye Uwanja wa Wembley, London, mabao ya Swansea yalifungwa Dyer na de Guzman (kila mtu alipachika mawili) na moja akafunga Michu.
Kituko kilitokea ni Dyer na Guzman kugombea kupiga mkwaju wa penalti, Dyer alitaka kukamilisha hat-trick lakini mwisho mwenzake ndiye akapewa kazi hiyo ya kuukwamisha mpira wavuni.

 de Guzman (kulia) na Dyer wakigombea penalti..

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic