February 25, 2013





Mara baada ya Simba kulala kwa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar, taarifa za kuachia ngazi kwa mwenyekiti wa klabu hiyo kongwe, Ismail Aden Rage zilienea kama moto wa petrol.

Taarifa hizo zilieleza Rage alikuwa ameamua kuachia ngazi baada ya kuona mambo yanazidi kwenda mlama.

Hata hivyo, alipozungumza na Salehjembe, Rage aliruka na kusema hakuna mtu ambaye amezungumza naye kuhusiana na hilo.

“Kama kuna mtu kakuambia nimefanya hivyo basi muamini yeye, sina taarifa hizo,” alisema Rage na alipoambiwa amefanya mahojiano na waandishi, akajibu:

“Sijazungumza na mwandishi yoyote kuhusiana na kujiuzuru, hapa unavyoona nimeitisha kikao cha kamati ya utendaji Jumatatu (leo), sasa nitaachia vipi ngazi halafu niitishe kikao.

“Ndiyo maana nakuambia sijazungumza na mtu yoyote, kwa kifupi naona mambo hayaendi vizuri na kuna watu wanatusakama, kuna njama tunafanyiwa, hii si hali ya kawaida,” alilalama Rage.

Askari Polisi walilazimika jana kuwaondoa kwa nguvu uwanjani mashabiki wa Simba ili kuepusha vurugu wakati wao walidai walitaka kukutana uso kwa uso na Rage na makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’.

Mashabiki hao walikuwa wakilalama kwamba uongozi mbovu ndiyo unaowafanya wayumbe na kufungwa katika mechi ya jana dhidi ya Mtibwa Sugar.

2 COMMENTS:

  1. Bora akae pembeni tu maana hali ishakuwa si hali kwenye timu na mwenendo ni mbovu hasa sasa asisubiri mpaka wamvunjie heshima kwake....

    ReplyDelete
  2. Hata tabora tu hawamtaki hahahahahahaha

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic