March 11, 2013



Na Saleh Ally
KOCHA Mkuu wa Yanga, Ernie Brants amesema pamoja na wachezaji wake kushindwa kufunga bao zaidi ya moja katika mechi tatu mfulizo, lakini timu nyingi zinacheza mchezo wa kujilinda zaidi.

Brandts amesema Yanga imekuwa ikitahidi kutaka kushinda, inacheza soka la kuvutia pamoja na kutafuta ushindi wakati wapinzani wao wanakaa nyuma tu.
“Ukiangalia mechi na Azam FC, asilimia kubwa wachezaji wao walikuwa wamekaa nyuma na kushambulia kwao ni kwa kushitukiza. Baadaye tulichezana Kagera Sugar, basi mambo yalikwenda hivyo hivyo.

“Nilifikiri katika mechi na Toto kungekuwa na mabadiliko kidogo, lakini mambo yalishindikana kabisa, utaona timu imejaza wachezaji wote nyuma, nafikiri si kitu sahihi,” alisema Brandts.

“Nafikiri soka la Tanzania linapaswa kuwa la ushindani ili kupiga hatua, lakini aina ya uchezaji ule, hauwezi kuwa sahihi. Tutaharibu mpira wa Tanzania na mambo hayatakuwa mazuri, waambieni.

“Ushindani ni pamoja na kucheza soka la ushindani, ndiyo maana umeona kuna makocha wamekuwa wakilaumiwa na kuitwa wanaharibu soka, wanacheza mpira wa kukaa nyuma tu bila ya kushambulia na kupanga uchezaji ambao pia unaweza nkuwavutia mashabiki. Hali hii inaniumiza sana.”

 Mara nyingi, Brandts aliyewahi kuichezea timu ya taifa ya Uholanzi, amekuwa akisisitiza anataka timu yenye uwezo wa kucheza soka la kujvutia, kushambulia mfululizo na kufunga mabao mengi.

SOURCE: CHAMPIONI      

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic