March 10, 2013




Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts amewaambia washambuliaji wake bado haridhiki na kiwango cha ufungaji mabao.

Yanga ina washambuliaji nyota kama Jerry Tegete, Didier Kavumbagu, Saidi Bahanuzi na Hamis Kiiza ambao wanaonekana kuishiwa mafuta ya kupachika mabao kwa kipindi sasa.

Brandts, beki wa zamani wa timu ya taifa ya Uholanzi iliyocheza hadi Kombe la Dunia, amesema hali ya wachezaji wake kutotumia nafasi za kufunga wanazozipata inamchanganya.


“Hili si tatizo la siku moja iliyopita, tumelizungumza sana na mara nyingine kulifanyia mazoezi.

“Lakini inaonekana bado, nafikiri sitalaumu kama nilivyosema lakini tutaendelea kulifanyia kazi kwa kwua nataka Yanga inayofunga mabao zaidi ya matatu kila mechi ikiwezekana.

“Bado nina washambuliaji wazuri kabisa ambao wanaweza kufanya hivyo, ndiyo maana inanichanganya kwa kiasi fulani,” alisema Brandts.

Yanga imekuwa ikishinda bao 1-0 kila mechi inayocheza katika kipindi ambacho inahitaji kujikita zaidi kileleni.

Hata hivyo, mwendo wake wa kuchota pointi tatu kila mchezo, unaonekana kuisaidia zaidi ingawa kweli inahitajika kufunga mabao zaidi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic