March 10, 2013




Baadhi ya wachezaji Simba huenda wakapata maisha nchini Oman kutokana na kuendelea kufuatiliwa na wakala nchini humo.

Said Al Maskery ambaye ni mmoja wa mawakala maarufu nchini Oman, amesema amekuwa akiendelea kuwafuatilia baadhi ya wachezaji wa Simba.

Hivi karibuni, Simba iliweka kambi ya wiki mbili nchini humo kujiandaa na Ligi Kuu Bara na michuano ya kimataifa.


Akizungumza moja kwa moja kutoka jijini Muscat, Oman, Al Maskery alisema kuna baadhi ya wachezaji hasa ambao ni chipukizi, anaendelea kuwafuatilia na usajili utakapofunguliwa ataangalia cha kufanya.

“Kweli kuna wachezaji tunawafuatilia taratibu kwa kuwa sasa tuna muda wa kutosha kabla ya kuanza usajili na tumeanza kufanya hivyo kitambo. Kwa sasa sitawataja majina,” alisema.

“Kama tutaridhika, basi tutafanya mazungumzo na Simba, pia mchezaji kwa ruhusa ya klabu. Baada ya hapo klabu inayowataka nayo itafuata taratibu kwa muongozo,” alisema.

Al Maskery ambaye amewahi kuwapeleka wachezaji kadhaa wa Simba nchini Oman tokea miaka ya 1990, alisisitiza, zaidi amekuwa akiangalia wachezaji makinda ingawa wakati mwingine suala la mahitaji ya timu linampelekea kutafuta mchezaji fulani.

Wakala huyo amekuwa maarufu sana kwa kuwatafutia wachezaji timu lakini pia makocha mbalimbali ambao wako chini ya kampuni yake.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic