March 8, 2013




Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts amesema analala kwa shida kubwa, anashindwa kupata usingizi mzuri kutokana na kutaka kupanga namna ya kuona wafungaji wake wanabadilika.

Brandts raia wa Uholanzi amesema washambuliaji wake wamekuwa wakipoteza nafasi nyingi sana za wazi, kitu ambacho ni hatari kwake.


Amesema mara kadhaa amekuwa akifanya mazoezi na kikosi chake kuhakikisha kinatengeneza nafasi nyingi za kufunga lakini mambo yanaonekana kuwa tofauti kabisa.

“Mara nyingi nimesikia watu wakisema au magazeti kwamba mimi nawalaumu wafungaji wangu, siwezi kufanya hivyo kwa kuwa kulaumu si njia nzuri ya kutatua tatizo. Nafikiri hujawahi kuniona hata nikilaumu wachezaji uwanjani.

“Nakosa usingizi mzuri, maana nataka kuona wanafunga kwa sababu wana uwezo wa kufanya hivyo. Tunatengeneza nafasi nyingi sana za kufunga lakini hatuzitumii.
“Ukiangalia nina washambuliaji bora kabisa, Tetege, Saidi (Bahanuzi), Didier (Kavumbagu) na Hamis (Kiiza), tunastahili kuwa na mabao mengi zaidi.

“Utaona mazoezi ya leo tunachofanya ni namna ya kufunga, krosi za juu na chini. Namna ya kutulia, ingawa bado tunapata shida kutokana na uwanja wenyewe,” alisema Brandts.

Kavumbagu ana mabao tisa, wakati Jerry aliyeibuka katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara, ana mabao saba. Washambuliaji hao wamekuwa wakipoteza nafasi nyingi za kufunga.

Katika mechi mbili zilizopita za Yanga, walipoteza zaidi ya nafasi kumi na kiungo Niyonzima ndiye aliwaokoa kwa kufunga katika mechi hizo dhidi ya Azam FC na Kagera Sugar ambazo Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0 kila mechi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic