March 7, 2013


Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ ametangaza kuachia nafasi yake hiyo.
Kaburu ameamua kuachia ngazi ikiwa ni saa chache baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Pope kubwaga manyanga.

Habari za Kaburu kujiuzulu zimethibitishwa na uongozi wa Simba, ingawa mwenyewe hakupatikana kulizungumzia hilo.
Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala amethibitisha hilo jana alipozungumza na Blog namba moja ya michezo nchini Tanzania ya Salehjembe.

“Ni kweli Kaburu amejiuzulu na tayari tumeshaueleza umma kuhusiana na hilo, amechukua uamuzi huo na kutoa taarifa kwetu,” alisema Mtawala.

Kuondoka kwa Hans Pope na Kaburu ambao wote ni wajumbe wa kamati ya utendaji ya Simba, kunamuweka Mwenyekiti, Ismail Aden Rage katika wakati mgumu.
Kutokana na mwenendo wa Simba, Rage amekuwa akishinikizwa kujiuzulu, ingawa amekuwa mgumu kama ‘nyundo’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic