March 8, 2013


Domayo (kushoto) akiwania mpira na Nurdin ambaye pia anatakiwa kufanyiwa upasuaji wa goti ndani ya wiki hii...
Kiungo kinda wa Yanga, Frank Domayo sasa ana jina jipya ambalo limetokana na uwezo mkubwa wa kupiga pasi anapokuwa anakichezea kikosi hicho.

Domayo amekuwa akipiga pasi za uhakika anapocheza katika mazoezi ya timu hiyo, lakini amekuwa bora zaidi katika mechi za Yanga.


Kutokana na kuonyesha uwezo huo, wenzake wamembandika jina la chumvi, wakiwa na maana ndiye anayenogesha mambo kama kiungo chumvi katika mboga.
Awali ilikuwa kazi kuelewa maana ya chumvi kutokana na maneno mengi ya Kiswahili kubadilishwa maana na vijana wa mjini.

Lakini baadaye wachezaji hao walifafanua kuwa chumvi imetokana na uwezo huo wa kupiga pasi safi zenye ‘macho’.

Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts naye alijikuta akiungana na wachezaji wake na kumuita jina hilo.
Wakati Domayo ambaye ni mtaratibu akiondoka mazoezini, Brandts alimuita: “Chumvi, how are you.” Hali iliyosababisha watu waliokuwa eneo hilo waanze kucheka.

Pamoja na kuwa kinda, Domayo tayari ni tegemeo kwa Yanga na Taifa Stars, yote inatokana na uwezo mkubwa na utulivu wake uwanjani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic