April 28, 2013



Klabu ya Manchester United iko katika hatua za mwisho za kumnasa mshambuliaji wa Borussia Dortmund, Robert Lewandowski kwa kitita cha pauni milioni 25.

Tatizo kubwa wapinzani wa Dortmund, Bayern Munich nao wametoa dau sawa na la Man United hivyo kufanya mchezo uwe mgumu. 

Kocha Mkuu wa Man United, Alex Ferguson ambaye amekuwa akimuwania mchezaji huyo kwa miezi 18 sasa, anataka kumtumia raia huyo wa Poland kama pacha wa Mholanzi, Robin van Persie iwapo kila kitu kitakwenda safi.


Mabao yake manne dhidi ya Real Madrid katika mechi ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa imezidisha nguvu ya timu hizo mbili kuhakikisha zinamnasa kwa ajili ya msimu ujao.

Mashabiki wa Dortmund wanaona ni bora mshambuliaji huyo kama atatua man United kuliko kwenda kwa wapinzani wao hao ambao tayari watamchukua mshambuliaji wao mwingine machachari, Mario Gotze kwa kitita cha pauni milioni 23.

Hata hivyo, United wamekuwa na hofu huenda Lewandowski akaamua kubaki Ujerumani na kutua Bayern kwa kuwa kuna taarifa za kusaini mkataba wa awali na klabu hiyo ya Magharibi mwa Ujerumani.

Suala la mashabiki wa Dortmund kutokuwa na furaha kama Lewandowski atabaki na kucheza Bayern ndiyo imekuwa silaha ya Ferguson akisisitiza bora angecheza nje ya Ujerumani kuepuka kuwaumiza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic