April 28, 2013




Pamoja na kuangushwa, Amir Khan ameonyesha yeye ni mpambanaji hasa baada ya kuinuka na baadaye kumshinda kwa pointi Julio Diaz.


Katika pambano hilo lililochezwa usiku wa kuamkia leo, Khan mwenye miaka 26 amefanikiwa kumtwanga Diaz ambaye alimuangusha katika raundi ya nne na kupoteza matumaini ya mashabiki wa Mwingereza huyo.


Baada ya Khan kuangushwa, mashabiki wake walijua mambo yangeendelea kuwa mabaya kama ilivyokuwa katika mapambano mawili yaliyopita dhidi ya Lamont Peterson na Danny Garcia ambayo yote alipoteza.

Baada ya kuinuka, Khan ambaye hiyo ni mechi yake ya pili chini ya kocha mpya, alionyesha kubadilika na kupigana kwa kushambulia zaidi huku ngumi zake nyingi zikimpata Diaz.


Wakati wa matokeo yanatangazwa, bado mashabiki wa Khan walionekana hawana uhakika kama alikuwa ameshinda kwa hofu ya kuangushwa katika raundi ya nne.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic