April 28, 2013



Kiungo nyota wa Yanga, Athumani Iddi ‘Chuji’ amesema jezi namba 24 imekuw ana baraka kubwa kwake baada ya kufanikiwa kutwaa ubingwa akiwa anaitumia.

Ukiachana na hivyo, Chuji amesema namba hiyo imemsaidia kucheza vizuri katika msimu unaomalizika Mei 18 pamoja na kwamba wengi waliamini haitawezekana.


“ Wakati nimerudi Yanga, wengi hawakuamini kama nitacheza vizuri nikiwa natumia zaidi ya namba nne ambayo nilikuta anaivaa Oscar Joshua.

“Lakini nikawaambia waniamini, sasa nimefanya vizuri. Ninashukuru sana kwa kuwa ulikuwa msimu mzuri kwangu,” alisema Chuji.

“Naichukulia namba ishirini na nne kama moja ya namba yenye bahati kwangu, nitaendelea kuitumia jezi hii.”

Yanga imefanikiwa kutwaa ubingwa ikiwa na mechi mbili mkononi na mchango wa Chuji umekuwa mkubwa katika kikosi hicho cha Jangwani.

Chuji amekuwa tegemeo katika kiungo cha ukabaji maarufu kama duara la chini, lakini amekuwa akishirikiana vema na Haruna Niyonzima raia wa Rwanda kuichezesha timu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic