April 28, 2013



Barthez..
Benchi la ufundi la Yanga, limechukua uamuzi wa kuwapumzisha wachezaji wake wenye kadi mbili za njano kutocheza katika mechi ya Jumatano dhidi ya Coastal Union.

Yanga inaivaa Coastal Union katika mechi yake hiyo ya pili kabla ya kumaliza msimu na Kocha Mkuu, Ernie Brandts amepitisha suala hilo.
Wachezaji wa Yanga wenye kadi mbili za njano ni Ally Mustapha ‘Barthez’, David Luhende, Didier Kavumbagu, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva na Hamis Kiiza.
Kiiza...

Brandts amechukua uamuzi huo kutokana na kuhofia wanaweza kulambwa kadi nyingine ya njano halafu wakaikosa mechi ya mwisho ya ligi dhidi ya Simba.

Kutokana na uamuzi huo, huenda Yanga ikaonekana na kikosi tofauti katika mechi hiyo ya Jumatano.

Haijajulikana kama anaweza kumtumia mchezaji mmoja au wawili kati ya hao sita.

Lakini golini ataanza Said Mohammed ambaye amekuwa hapati nafasi ya kutosha kutokana na umahiri wa Barthez langoni unaomfanya apate nafasi ya kuwania tuzo ya kipa bora wa msimu wa 2012-13.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic