April 13, 2013




Ujumbe wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) utakaowasili nchini keshokutwa utaongozwa na Primo Corvaro.

Corvaro ndiye anaonekana kukabidhiwa masuala yote ya migogoro na shirikisho hilo hasa kwa upande wa bara la Afrika.

Imeelezwa Corvaro ndiye amekuwa akishughulikia migogoro yote inayojitokeza katika nchi za Afrika badala ya Ashford Mamelodi kama ilivyokuwa imezoeleka awali.

Hata hivyo, kabla ya kukabidhiwa mikoba hiyo kutoka kwa bonge la mtu, Mamelodi, Corvaro alilazimika kusoma taratibu mambo mengi kuhusiana na sola la Afrika pamoja na siasa inavyochukua nafasi kubwa.

Imeelezwa Mamelodi anatarajia kustaafu baada ya miaka michache, hivyo Corvaro ndiye atachukua nafasi yake.

Ndiyo maana katika masuala ya migogoro katika nchi kadhaa, Carvaro alilazimika kusafiri na Mamelodi ili kujua mambo kadhaa yanavyokwenda.
Walikuwa pamoja nchini Uganda, Februari mwaka jana kutatua mgogoro wa ligi ya soka nchini humo ambao ulidumu kwa zaidi ya miezi miwili.

Mwaka jana hiyohiyo, Corvaro alifanya kazi ya kubwa ya kumaliza suala la mgogoro mwingine wa kisoka nchini Sierra Leone.

Corvaro ndiye ataongoza timu itakayotua nchini Jumatatu, tayari kumaliza suala la mgogoro wa uchaguzi mkuu wa TFF kwa kuwaona wagombea na kuwasilikiza, hasa wale ambao wana madai ya kutotendewa haki na kuenguliwa katika mchakato wa uchaguzi au vinginevyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic