April 23, 2013

 
Baada ya Manchester United kutwaa taji la 20 la ubingwa wa Ligi Kuu England, beki wake Patrice Evra ameherekea kwa staili ya aina yake inayoonekana kumdhihaki mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez.


Evra alionekana akishangilia akiwa na kipande cha mkono, dakika chache baada ya Man United kuichapa Aston Villa na kubeba ubingwa.


Suarez ndiye gumzo katika soka ukiachana na ubingwa huo wa Man United, ikiwa ni kutokana na kitendo chake cha kumng’ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic.


Evra na Suarez waliwahi kuingia katika mgogoro miezi kadhaa iliyopita baada ya Mruguay huyo kutuhumiwa kumtolea Evra maneno ya kibaguzi.
Suarez alikumbana na adhabu ya kufungiwa kucheza mechi nane pamoja na kupigwa faini ya noti za ‘malkia’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic