April 23, 2013



Kocha Mkuu wa Kagera Sugar, Abdallah ‘King’ Kibadeni amesema makocha wazawa wanaweza kuleta mabadiliko.

Kibadeni aliyewahi kuwa mshambuliaji hatari wa Simba, amesema makocha wazawa wameonyesha wana uwezo mkubwa katika msimu huu wa ligi.


Hivyo kuna kila sababu ya viongozi wa klabu mbalimbali kuangalia suala la kuwapa nafasi.

“Angalia Kagera, tunakwenda vizuri na Mtibwa Sugar na Coastal bado zina nafasi nzuri ya kuendelea kupata pointi katika mechi za ligi.

“Lakini Yanga imecheza na Mugambo na kupata wakati mgumu sana, ukilinganisha anacholipwa kocha wa timu hiyo na wachezaji wao na wale wa Yanga kuna tofauti kubwa.

“Kama makocha wazawa wakipewa nafasi na kuaminiwa, wakalipwa vizuri zaidi huku wakifanyiwa usajili mzuri, basi wanawea kufanya vizuri kuliko makocha wa kigeni.

“Tuwaamini kwa kuwa wanajua mengi kuhusiana na soka letu na wengi wapo wenye utaalamu ingawa sina maana makocha wageni wasije nchini.”

Kibadeni ndiye kocha mwenye rekodi nzuri zaidi kwa upande wa klabu kwa kuifikisha Simba katika fainali ya Kombe la Caf mwala 1993 lakini ikapoteza mjini Dar es Salaam kwa kufungwa mabao 2-0 dhidi ya Stella Abidjan ya Ivory Coast.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic