April 27, 2013




Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji amesema amefurahishwa na Yanga kutimiza moja ya malengo yake makubwa kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara, lakini haoni kama kuna sababu ya kufanya sherehe kubwa.

Akizungumza moja kwa moja na Salehjembe kutoka nje ya Tanzania, Manji alisema ubingwa ni sehemu ndogo tu ya malengo wanayotaka kufikia.


“Tunaweza kusherekea lakini si kufanya sherehe kubwa ambayo itatugharimu fedha nyingi sana. Tunahitaji fedha kwa ajili ya kujenga uwanja, ni fedha nyingi mno.

“Hivyo haitakuwa jambo la busara kutumia fedha nyingi kufanya sherehe. Lakini bado nawapongeza viongozi wenzangu, benchi la ufundi, wachezaji na Wanayanga wote kwa ujumla.

“Umoja na ushirikiano wetu umetufanya tufike hapa lakini bado tuna safari ndefu na tunapaswa kuudumisha ili tuendelee kufikia malengo tuliyojiwekea,” alisema Manji.

Yanga imetawazwa kuwa bingwa jana saa 12:30 jioni baada ya mechi kati ya Coastal Union na Azam kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Baadhi ya mashabiki wa Yanga walikuwa wakitaka kufanyika kwa sherehe kubwa baada ya wao kufanikiwa kutwaa ubingwa huo.

Maana yake, kama itawezekana, itafanyika sherehe ndogo tu au haitakuwepo kabisa kutokana na maelezo ya mwenyekiti wao ambaye anaangalia kusonga mbele zaidi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic