April 27, 2013



Ingawa kasi yao bado haijawa kubwa, lakini baadhi ya wajumbe wa kundi maarufu la Friends of Simba wameanza kusaidia kazi kadhaa ndani ya klabu hiyo.

Wajumbe hao wameanza kuhaha katika baadhi ya sehemu kuhakikisha kikosi cha Simba kinabadilika msimu ujao.

Taarifa za uhakika ambazo Salehjembe inazo, wajumbe hao wamekuwa wakizungumza na wachezaji kadhaa kuhakikisha wanajiunga na Simba ili kujenga kikosi imara cha msimu ujao.


“Kweli baadhi tumerudi na kuanza kusaidia kazi za usajili na nyinginezo, klabu iko taabani kifedha na utaona mambo mengi ni magumu.

“Lakini kuna baadhi wanahofia kuingia moja kwa moja kwa kuwa hawamuamini mwenyekiti, maana anaweza kusema anataka ushirikiano katika wakati mgumu lakini baadaye akageuka.

“Hivyo wanataka uhakika wa mambo zaidi, ndiyo maana wako pembeni kidogo. Lakini wakiona kuna ukweli basi timu nzima itarudi,” kilieleza chanzo cha uhakika kutoka katika kundi hilo.
Friends of Simba ndiyo kundi maarufu zaidi linaloogopewa kwa kusuka timu pamoja na mipango ya ushindi katika soka Tanzania.

Kuondoka kwa kundi hilo ambalo Mwenyekiti wake ni Zacharia Hans Pope, kuliifanya Simba iyumbe ingawa angalau kwa msimu mmoja, ilifanya vizuri. Lakini msimu huu, Simba ikawa dhoof-li hali.

Uongozi wa Simba chini ya Ismail Aden Rage uliokuwa ukitangaza kwamba kundi hilo linawahujumu, hivi karibuni ulikwenda kupiga magoti na kukiri mambo ni magumu.

Wako wajumbe wamekubali kurudi na kushirikiana naye, lakini wengine bado wana hofu kwamba mara nyingi hakuna kauli dhabiti zinazosemwa na uongozi huo wa Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic