April 21, 2013



FULL TIME
Dk 5 za nyongeza.
Dk 87, Dihile anaokoa shuti kali la Nizar na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda

Dk 80, Ruvu wamepotea, Dihile anafanya kazi ya ziada kuokoa shuti kali la Nizar


Dk 73, Dihile anafanya kazi ya ziada kumzuia Msuva baada ya kupokea pasi ya Niyonzima.
Dk 68-71 Yanga wanafanya mashambulizi mfululizo lakini wanakosea katika kumalizia.






GOOOOOOO..Dk 64 Nizar anaifungia Yanga bao la tatu baada ya kufanya shambulizi kali na Domayo kupiga mpira uliogonga mwamba na kumkuta mfungaji.


GOOOOOOOO..Dk 58 Kiiza anaifungia Yanga bao la kichwa baada ya krosi safi ya mpira wa faulo ya David Luhende

Dk 52, Kiiza katika nafasi nzuri huku mabeki wa Ruvu wakidhani ameotea, anapiga shuti kuuuuubwaaaaa juu.
Dk 50, Cannavaro anaokoa shuti la Mgisa na kuwa kona ambayo barthez anaihifadhi.
Dk 46, nizar anawatoka mabeki watatu na kupita shuti linalotoka sentimeta chache pembeni

HALF TIME:
Baada ya filimbi ya mapumziko, wachezaji wa Ruvu wanaanza kuzozana katikati ya uwanja kabla ya kuingia vyumbani.



GOOOOOOOOOOO Dk 45, Msuva anaifungia Yanga bao baada ya kuuwahi mpira wa kurusha huku mabeki wa Ruvu wakidhani ameotea na mwamuzi Oden Mbaga anasema, “weka kati”.
Dk 42, Ruvu wanaonekana kupoteza muda kama wanahitaji sare
DK 37, Pazi anapoteza nafasi nyingine kwa kushindwa kuupiga mpira
Dk 35, lango wazi la JKT, Kiiza anapiga shuti nje.
 Dk 32, Mgosi anapiga shuti kali baada ya kumtoka Yondani, lakini halikulenga goli.
Dk 31 Msuva anapiga shuti kali linalogonga mwamba na kurudi uwanjani.
Dk 30, Nizar anawapiga chenga mabeki wa Ruvu na kuachia shuti la chini, Dihile anatoa na kuwa kona.


Dk 25, Pazi anapiga shuti safi baada ya kumhadaa Twite lakini linatoka nje
Dk 24, Mgosi anawahadaa mabeki wa Yanga na kupiga shuti hafifu linalodakwa kilahisi
Dk 22, mpira wa faulo wa Luhende unatua kichwani mwa cannavaro, unatoka sentimeta chache.
Dk 21, krosi ya Twite, kipa dihile anafanya kazi ya ziada kuokoa mpira kichwani mwa kiiza.


Dk 19 Chuji anapoiga shuti kali linatoka sentimeta chache.
Dk 16, pasi nzuri ya Nizar, mita tatu kutoka langoni Kiiza anapiga shuti lakini beki Makwaya analala na kuokoa, inakua kona tasa.
Dk 12 Makwaya anapiga shuti hafifu baada ya pasi nzuri Mgosi, kipa Barthez analidaka kwa ulaiiniii.



Dk 9, Nizar anageuka na kupiga vizuri baada ya kuwahadaa mabeki wa Ruvu lakini anashindwa kulenga lango
Dk 7, shuti kali ya Twite linapita juu ya lango ilikuwa ni baada ya pasi nzuri ya Msuva.
Dk 5, Dihile anaikuka na mechi inaendelea
DK 1-3, Yanga wanapata kona tatu ambazo zote zinakuwa tasa ni baada ya kufanya mashambulizi mfululizo. Kipa wa JKT, Dihile yuko chini baada ya kugongana na Nizar.
Mpira umeanzam Yanga inapeleka mashambulizi kaskazini na Ruvu kusini.
RUVU JKT:
Dihile, kikutwa, nkomola, madenge, makwaya, naftary, mgisa, mkanga, mgosi, pazi na adolf (C)
YANGA:
Barthez, twite, luhende, cannavaro (C), yondani, chuji, msuva, domayo, kiiza, nizar na niyonzima

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic