April 19, 2013



van Persie

Mwandishi Wetu
NAJUA makala hii inaweza kuzusha ubishi mkubwa hapo ulipo kama utakuwa na wenzako ambao ni wadau wa soka pia, wapo wanaodai kuwa kufunga bao kwa penalti ni bahati, lakini wengine wanaamini uwezo wa kupiga penalti nao unachangia.

Kuna wachezaji wengi wenye uwezo wa kupiga penalti duniani, wafuatao wanatajwa na wengi kuwa uwezo wao ni mkubwa zaidi ya wengine;

Robin Van Persie
Staa wa Man United ana uwezo mkubwa kwa kutumia mguu wa kushoto kupiga penalti, yeye na Wayne Rooney ndiyo wenye jukumu hilo klabuni hapo.

Graham Alexander
Beki wa pembeni ambaye hakuwa na jina kubwa, baadhi ya timu alizopita ni Burnley na Preston North End zote za England.
 
Balotelli
Mario Balotelli
Anaonekana kama ‘chizi’ lakini akisimama mbele ya 18 anajua wapi pa kupiga, kwa sasa anaichezea AC Milan.

Baines

Leighton Baines
Beki wa kushoto wa Everton ambaye pindi anapopiga penalti kwa mguu wake wa kushoto ni vigumu kukosa.
 
Cruff..
Johan Cruyff
Alikuwa kocha mwenye mbinu nyingi lakini enzi zake za uchezaji pia alikuwa mbunifu wa penalti. Jina lake litaendelea kukumbukwa daima kutokana na mchango wake katika soka.

Gerd Muller
Ataendelea kukumbukwa siku zote nchini Ujerumani kutokana na uwezo wake wa kufunga, Muller aliweza kufunga penalti nyingi katika maisha yake ya soka.

Ronaldinho
Enzi zake alikuwa mwepesi na mjanjamjanja awapo na mpira.

Gary McAllister
Alicheza klabu nyingi lakini akiwa Liverpool alipata heshima kwa kuwa alikuwa na uzoefu zaidi. Aliwahi kukosa penalti muhimu katika michuano ya Ulaya 1996 alipokuwa akiichezea Scotland dhidi ya England.

Eric Cantona
Aliyekuwa kijana mtukutu lakini mbele ya lango hakuwa na utani kabisa, alifunga penalti nyingi pia.

Andrea Pirlo
Mashabiki walioshuhudia michuano ya Euro 2012 wanajua ‘muziki’ wake, alipiga penalti akiwa kwenye kikosi cha Italia kilipocheza dhidi ya England, ambapo alikuwa kama anapiga shuti kisha akapiga taratibu huku akimuacha kipa Joe Hart ‘akipotea vibaya’.
 
Ballack
Michael Ballack
Kiungo wa Ujerumani ambaye alikuwa akicheza soka la nguvu, alikuwa na uwezo mzuri wa kupiga penalti, jukumu alilofanya akiwa klabuni na timu ya taifa.
 
Platini
Michel Platini
Rais wa sasa wa Uefa ambaye alisaidia Ufaransa kutwaa ubingwa wa Euro 1984, alikuwa na mbinu kali kila alipokwenda kupiga penalti.


Steven Gerrard
Nahodha mkongwe wa Liverpool ambaye wapo wanaomuita kwa jina la utani la Mr Liverpool, ana uzoefu wa kupiga penalti na amekuwa akipiga vizuri licha ya kuwa amewahi kukosa mara kadhaa.
 
Pirlo
Alessandro Del Piero
Aliifungua Juventus na timu ya taifa ya Italia mara nyingi.

Cristiano Ronaldo
Amefunga mabao mengi kwa njia ya penalti, siyo mtaalam sana ila ni nadra kukosa, amefanya vizuri akiwa Man United, Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno.

Frank Lampard
Kiungo mkongwe wa Chelsea ambaye jukumu la kupiga penalti anapewa yeye.

Zinedine Zidane
Kitendo cha kumpiga kichwa Marco Materazzi mwaka 2010 kinakumbukwa zaidi, lakini wanaomfuatilia wanajua alivyokuwa bora kwenye penalti.


Alan Shearer
Nguli wa Newcastle ambaye alikuwa na uwezo mkubwa wa penalti.

Matthew Le Tissier
Hajulikani kwa kiwango cha juu, aliwahi kukosa penalti moja tu kati ya 43 alizopiga katika maisha yake ya soka la kulipwa. Tissier, 44, aliichezea Southampton kuanzia mwaka 1985 mpaka 2002 na kufunga mabao zaidi ya 161. Bahati mbaya ni kuwa aliichezea timu ya taifa mechi nane tu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic