April 23, 2013

Angalia picha hii utapata funzo kubwa sana, hiki ni kikosi cha Simba miaka minne iliyopita.

Ukihesabu utaona wachezaji waliopo ni 26, pamoja na viongozi wanne walio katika picha hii.

Ukitaka kujua timu zetu za Tanzania zinabahatisha mambo mengi, ngoja nikupe ufafanuzi wa hili linalofuata.


Ndani ya miaka minne tu, kati ya wachezaji hao 26 walio katika kikosi cha Simba msimu huu ni wachezaji sita tu. Maana yake 20 wote walishaondoka ndani ya miaka hiyo.

Hao sita waliobaki ni Juma Kaseja, Ramadhani Shamte, Juma Nyosso, Haruna Moshi ‘Boban’, Amri Kiemba na Ramadhani Chombo ‘Redondo’.

Katika hao sita waliobaki, wenye uhakika wa kucheza katika kikosi kilicho chini ya Mfaransa ni wawili tu, Kaseja na Kiemba. Upande wa Shamte, yeye ni mtu anayetafuta namba.

Wengine watatu, yaani Nyosso, Redondo na Boban wao wamesimamishwa kwa madai ya utovu wa nidhamu sasa takribani mwezi.
Lakini hadi leo uongozi na benchi la ufundi wamekuwa wakitupiana mpira kila upande. Maana uongozi unasema utaliambia benchi la ufundi litoe maelezo lakini hadi sasa haujatoa.

Si kitu lahisi, benchi la ufundi likamsimamisha mchezaji lakini lisitoe maelezo kwa uongozi kwa zaidi ya mwezi na mshahara mchezaji anaendelea kuchukua.

Hali hii inaonyesha kuna mambo mengi sana ya kubabaisha, huenda uongozi ni tatizo lakini pia wachezaji wanaweza wakawa wanaguswa.

Ndani ya misimu mitano, wachezaji 26 waliopo ni sita tu na kati yao hao, wanaocheza ni wawili tu na wengine hawana nafasi.
Unaweza kusema wachezaji 24 hawana nafasi na wawili tu ndiyo wanaocheza.

Kwa upande wa viongozi wanne, wawili bado wanaendelea kubaki Simba ambao ni daktari Cosmas Kapinga na Amri Said ambaye yuko katika timu ya vijana.

Aliyekuwa Meneja, Innocent Njovu hayupo kama ilivyokuwa kwa Kocha Mkuu wakati huo, Patrick Phiri.

Kuna mambo mengi ya kuangalia, wachezaji lazima wadumishe viwango vyao lakini inaonekana suala la propaganda ya usajili linaziathiri timu.

Iko namna hii, kila unapofika wakati wa usajili, timu hutaka kuonekana magazetini na kwenye vyombo vya habari imefanya usajili wa kutisha.
Hivyo wanasajili hovyo, wanaacha wachezaji hovyo na hakuna uvumilivu hata kidogo.

Kama kuna mchezaji alifanya kosa moja katika mchezo fulani wa ligi, bila ya kuamini soka lazima liendane na makosa, basi anaondolewa mara moja na timu inafanya usajili wa kumchukua mchezaji ambaye huenda kiwango kinaendana tu au aliyesajiliwa anakuwa na kiwango cha chini zaidi.

TAFAKARI…NDIIIIIIII!

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic