April 23, 2013




Ilionekana ni kama kitu cha ajabu, lakini ndiyo hali halisi, si hadithi. Bayern Munich imeifunga Barcelona kwa mabao 4-0 katika mechi ya kwanza ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Barcelona pamoja na kuwa na Lionel Messi imejikuta inaogelea kipigo hicho cha aibu mjini Munich kwa kuchapwa mabao hayo.



Wajerumani hao wangeweza kushinda hata mabao saba, lakini mpira ndivyo ulivyo.

Mabao ya Bayern iliyokuwa nyumbani yalifungwa na Muller aliyefunga la kwanza na la nne katika dakika ya 25 na 82.



Gomez alifunga la pili katika dakika ya 49 na mkali, Robben yeye alifunga la tatu.

Angalia picha za action namba Barca walivyokuwa wanapelekwa puta kama watoto wa ‘shule’.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic