April 26, 2013




Mke wa Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Liewig ametua jijini Dar es Salaam na kuungana na mumewe.

Mke huyo yuko nchini kwa zaidi ya wiki tatu akiishi na mumewe ambaye anaendelea kazi ya kuinoa Simba.

Pamoja na kukubali mkewe yuko Dar pamoja naye, lakini Liewig raia wa Ufaransa hakutaka kuzungumzia zaidi.

“Kweli yuko hapa, siku chache zijazo ataondoka lakini vizuri tukazungumzia mambo mengine,” alisema.

Hata hivyo, mambo yamekuwa hayaendi vizuri katika kikosi hicho cha Msimbazi kinachotumia vijana wengi zaidi.

Liewig ambaye alichukua nafasi ya Milovan, tayari amekubali kuwa kikosi chake hakina nafasi ya kuchukua hata nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu.

Yanga wameishatangazwa kuwa mabingwa, Azam FC imejihakikishia nafasi ya pili na Simba inaendelea kuwania nafasi ya tatu ikichuana na Kagera Sugar na Coastal Union.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic