April 26, 2013




Uongozi wa Yanga umetaka kupewa muda zaidi ili kuchagua ramani ya uwanja inaoutaka.


Awali uongozi wa Yanga ulitangaza kuwa siku saba tu zilikuwa zinatosha kabla haijachagua inataka ramani ipi kati ya tatu ilizopewa na kampuni ya Beijing Construction Engineering Group (BCEG) ya China.

Akizungumza kutoka China, Meneja wa BCEGC aliyejitambulisha kwa jina moja la David alisema mambo yanakwenda vizuri na wameamua kuwapa Yanga muda zaidi.


“Ni jambo la msingi wawe na muda zaidi ya kuchagua kutokana na uwezo wao, eneo lao na mambo mengi ya kitaalamu yanatakiwa.

“Tunajua wanalazimika kukutana na kujadili, wiki moja isingetosha, lakini hata wao wameona hivyo. Maana yake tunaenda vizuri,” alisema David ambaye alisema anarejea nchini baada ya siku chache.

BCEG iliyojenga Uwanja wa Taifa Dar, ilitoa ramani tatu kwa uongozi wa Yanga na kuwapa muda wachague moja kati ya hizo.

Katika ramani hizo za uwanja utakaojengwa kwenye Uwanja wa Kaunda jijini Dar, uwanja mkubwa una uwezo wa kuingiza watu 50,000 unafuatia unaobeba watu 40,000 na mwisho ni ule unaochukua watu 30,000.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic