April 19, 2013





Hatimaye sasa kila kitu hadharani baada ya kubainika walibuaji wa mabomu katika mbio za Boston Marathon ni ndugu raia wa Chechnya.

Tayari watu wausalama wa Marekani wameanza mapambano nao na kufanikiwa kumuua mmoja aitwaye Tamerlan Tsarnaev, 26, ambaye ni mkubwa lakini katika mapambano hayo askari polisi mmoja aliuwawa.


Mdogo wake  





Dzhokhar Tsarnaev, 19, ambaye amekuwa mtuhumiwa namba mbili bado anaendelea kutafutwa.

Kila kitu katika mji huo kimesimama kwa kuwa hakuna usafiri wa jamii kama mabasi na treni.


Raia wameambiwa wasimfungulie mtu wasiyemjua na ndege zimetakiwa kusitisha safari zake mara moja.

Taarifa za awali zinaeleza wawili hao wamekuwa wakiishi nchini Marekani tokea mwaka 2002 na miaka 11 baadaye ndiyo wametimiza walichokuwa wanataka kukifanya.

Tayari picha zao ziko mitaani na wananchi wameambiwa waendelee kutoa msaada wa kuhakikisha anapatikana wakati akiendelea kusakwa kila moja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic