April 15, 2013



 Mwenyekiti wa Kamati ya kusimamia jengo la klabu ya Yanga Ridhiwani Kikwete, leo ametaja kamati yake yenye watu nane itakayofanya kazi hiyo

Akizungumza katika mkutano maalum leo mchana katika Makao Makuu ya Klabu hiyo, Ridhiwani amewataja wajumbe hao ambapo Makamu wake atakuwa Issa Haji Usi kutoka Zanzibar huku pia akimjumisha Jaji Mkwawa kuwa mjumbe ambaye aliwahi kuwa naye katika kamati ya uchaguzi ya klabu hiyo.


Mbali na Mkwawa, wajumbe wengine ni Baraka Igangula ambaye ni mtaalam wa ramani za majengo, Allan Magoma, Mavale Msebo, Isaack Chanji na Charles Palapala huku wengine Beda Tindwa na Mahamoud Milandu ambao watakuwa nje ya kamati hiyo kuu wakiwa na kazi maalum ya kusaidia mawasiliano ya karibu na wadau watakaohitajika na kamati hiyo.

Ridhiwani amesema, lengo la kuchagua kamati hiyo iliyojaa wataalam mbalimbali wa mambo ya benki na ujenzi, ni kutaka kufanikisha majukumu hayo waliyopewa na Uongozi wa Yanga wa kulisimamia jengo hilo lililopo mtaa wa Mafia.

“Hii ni hatua ya awali kabisa, kwa kuanzia leo nimewataja hawa wenzangu ambao tutashirikiana kwa pamoja katika jukumu hili,kama kamati tutakuwa tunakutana mara kwa mara lakini sasa tunafikiria kuandaa vikao kama viwili mapema wiki ijayo ili tuweze kujipangia majukumu ya nani afanye nini,” alisema Ridhiwani

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic