April 15, 2013



 Kikosi kamili ya timu ya Yanga, kimeondoka leo mchana kuelekea Mkoani Tanga, tayari kuwafuata wenyeji wao JKT Mgambo.

Kikosi kamili cha Yanga kilichoondoka leo kikiongozwa na Kocha wao Mkuu Ernie Brandts kimewaacha nyota watano akiwemo Didier Kavumbagu aliyekumbwa na maumivu ya msuli wa kisigino huku wengine walioachwa na mabeki Juma Abdul,Stephano Mwasyika ambao nao bado wagonjwa.

Wengine walisalia jijini Dar ni Omega Seme na makinda watatu walipandishwa kutoka kikosi B Rehani Kibingu,George Banda na kipa Yusuph Abdul.


Kikosi kamili kilichowafuata Mgambo tayari kwa mchezo huo utakaopigwa keshokutwa katika Uwanja wa Mkwakwani ni pamoja na makipa Ally Mustapha ‘Barthez,’ Said Mohamed wakati mabeki wakiwa Nadir Haroub ‘Cannavaro,’ Kelvin Yondani, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, David Luhende, Godfrey Taita, Shadrack Nsajigwa ‘Fusso’ na Salum Telela.

Viungo ni Athuman Idd ‘Chuji,’Haruna Niyonzima, Nurdin Bakari, Frank Domayo, Hamis Kiiza, Nizar Khalfan, Simon Msuva huku washambuliaji wakiwa ni Said Bahanuzi na Jerry Tegete.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic