April 27, 2013




Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil itakuwa michuano ya kwanza ya soka kuonyeshwa katika mfumo wa Ultra HD.

Teknolojia hiyo tayari imeanza kutumika ingawa imeonekana kuwa ya wachache kutokana na televisheni zenye mfumo huo kuuzwa kwa bei ghali zaidi.


Mfano televisheni ya LG ya Ultra HD ya Inchi 84 inauzwa hadi pauni 20,000 (zaidi ya Sh milioni 52).

Lakini makampuni yanayotengeneza yameeleza kuanza katikati ya mwaka juu zitaanza kupatikana madukani hadi kuanzia pauni 5,000.

Lakini michuano hiyo ya Kombe la Dunia ndiyo itatumika kuitangaza zaidi teknolojia hiyo ambayo inaelezwa ubora wa picha zake ni mara nne kuliko unaoonekana katika televisheni za sasa.

Kwa upande wa Afrika inaonekana televisheni hizo huenda zikapata soko la chini kutokana na ukubwa wa bei kwa kuwa watakaonunua ni wachache walizonazo.

Hata hivyo, Waafrika wengi watakuwa na hamu ya kuzitumia huku waiweka matarajio yao makubwa kwa Mchina ambaye anaweza ‘kuchakachua’ na mambo yakaenda kama Ulaya tu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic