May 17, 2013



 
Arsenal imejadili suala la kutaka kumchukua mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney ambaye anaonekana kutokuwa na furaha.

Hata kabla ya mwaka mmoja baada ya kumuuza Robin van Persie kwa Manchester United, Arsenal imeona inaweza kumnasa Rooney ili kuongeza nguvu katika safu yake ya ushambuliaji.


Baada ya kikao hicho, inaonekana siku chache zijazo, Arsenal watakutana na wahusika wa United na kujadili suala la Rooney ambaye aliomba kuuzwa.

Lakini swali au mjadala mkubwa ni kiasi cha mshahara anacholipwa Rooney kwa wiki ambacho ni pauni 250,000 kama kweli Arsenal wataweza kukilipa.

Mfano mchezaji kama Lukas Podolski analipwa pauni 100,000 kwa wiki, hivyo huenda kukawa na ugumu kwa klabu hiyo ya London.

Kingine ni swali, kama kweli Rooney atakubali kwenda Arsenal ambayo imekuwa inaonyesha haina njaa ya vikombe.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic