May 17, 2013



Siku kama ya leo, Mei 17 inakumbukwa kama moja ya siku ya majonzi katika historia ya klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Simba wanaotumia rangi nyekundu na nyeupe, maarufu kama Wekundu wa Msimbazi walimpoteza kiungo wao, Patrick Mutesa Mafisango raia ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) katika ajali mbaya ya gari.


Gari lililosababisha kifo chake..

Gari hilo liligonga mti katika eneo la Veta Chang’ombe, mwendo wa dakika tatu kutoka nyumbani kwake Keko jijini Dar.

Alipata ajali hiyo wakati akitoka katika misele ya usiku na wenzake, inaelezwa alikuwa ‘maji’ wakati gari aina ya Toyota Cresta Mark II lilipomshinda na kugonga miti miwili.
 
Boban akisindikizwa na Said Kokoo kuingia mochwari

Boban akiingia mochwari na Kokoo, nyuma kaka yake Idd Moshi Myamwezi

Mafisango aliumia vibaya na kukimbizwa Muhimbili lakini ilikuwa vigumu kuokoa maisha yake. 

Ilikuwa usiku wa kuamkia Alhamisi Mei 17, 2012. Ndiyo leo, Mei 17,2013, Simba imetimiza mwaka sasa bila ya kiungo huyo.
 
Bondia Thomas Mashali, Emmanuel Okwi walifika Muhimbili asubuhi..

Niyonzima akiwa haamini baada ya kuuona mwili wa marehemu mochwari, kulia ni Uhuru Selemani aliyekuwa akilia kwa sauti ya juu

Simba itacheza mechi ya pili dhidi ya watani wake bila ya kuwa na Mafinsango, mechi ya kwanza ikiwa ni ile ya Oktoba 3, 2013 iliyomalizika kwa sare ya bao 1-1. Mechi ya mwisho Mafisango kuichezea Simba ilikuwa ni ile ambayo Wekundu wa Msimbazi walishinda kwa mabao 5-0.

Mashabiki wa Simba wanaendelea kumkumbuka Mafisango kutokana na umahiri wake wakati akiwa mchezaji wa Simba na msaada mkubwa aliokuwa akiutoa.
 
MAN FOR LOVE: Boban na Mafisango wakiwa wamekumbatiana, kulia ni Gervais Kago...
Ilielezwa Mafisango ndiye alitoa mchango mkubwa kwa kiungo Haruna Moshi ‘Boban’ kubadilika na kujali zaidi kazi yake.


Wakati akiwa Simba, Mafisango alikuwa rafiki wa karibu wa Boban na kwa kiasi kikubwa alimbadilisha na kumfanya arudi na kucheza soka.
Uthibitisho, hata wakati wa msiba, Boban ndiye alionekana kuguswa zaidi, alilia kutaka kuingia mochwari ili kuhakikisha kama kweli swahiba wake alifariki dunia.

Lakini aliomba ruhusa na kuondoka katika kikosi cha Taifa Stars, alisafiri hadi Kinshasa, DR Congo kwenda kumzika Mafisango.

Mafisango atakumbukwa kwa mengi ikiwamo utukutu wake, lakini uwezo mkubwa wa kusakata soka ndiyo unabaki kwua gumzo hadi leo.

RIP.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic