May 17, 2013




Pamoja  na kufanya ni siri kubwa, taarifa zinaeleza Mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga wanatarajia kuondoka Pemba leo jioni.

Imeelezwa Yanga watatua moja kwa moja mjini Bagamoyo tayari kujiandaa kuja Dar es Salaam kesho.

Wakiwa mjini Bagamoyo, Yanga watafikia katika hoteli ya kitalii na watapumzika hadi kesho watakapoanza safari ya kuja Dar es Salaam.


Mwandishi wetu wa Pemba amethibitisha hilo kwamba Yanga watatulia Bagamoyo kwa siku moja kabla ya kuanza safari ya kurudi Dar kesho tayari kwa mechi.

Kwa upande wa Simba, kikosi chao kinatarajia kutua na ndege leo jioni kikitokea Zanzibar.


Simba watalala Dar es Salaam, tayari kwa mechi hiyo ya kesho ambayo tayari ni gumzo kila sehemu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic