May 4, 2013




Kocha Mkuu wa Manchester City, Roberto Mancini ameingia hofu ya kazi yake baada ya uongozi wa klabu hiyo kukutana na wakala wa kocha wa Malaga, Manuel Pellegrini.
 
Pellegrini
Pellegrini amekuwa kati ya makocha waliokuwa wanatakiwa na Man City kwa kipindi kirefu sasa, lakini safari hii inaonekana wamepania kumchukua.

Mkurugenzi wa soka wa Man City, Txiki Begiristain alikutana na wakala huyo katika chakula maalum cha mchana jijini Madrid, siku chache zilizopita.

Pamoja na kuwa Mancini alihakikishiwa nafasi hiyo msimu ujao na Mwenyekiti wa Man City, Khaldoon Al Mubarak, bado ameonekana kuwa na hofu kutokana na mkutano huo wa Madrid.

 “Kiasi fulani inachanganya, ila siwezi kuwa na hofu kwa kuwa ndani ya msimu miwili tumepata vikombe vitatu. Mara moja mabingwa FA na ubingwa ligi kuu.


“Lakini angalia leo tuko katika nafasi ya pili na nachanganyikiwa kwa kuwa nilitaka kushinda ubingwa mwingine wa England. Lakini sijui, nafikiri swali hilo unaweza kumuuliza Txiki akafafanua vizuri,” alisema Mancini.

Hali hiyo inazidi kumpa hofu Mancini, lakini bado inaonyesha kocha huyo wa Mallaga anapewa nafasi ya kurejea Madrid kama Jose Mourinho ataondoka na kurejea Chelsea.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic