May 2, 2013



Luis Suarez ameonywa na mkewe na kutakiwa kubadilika mara moja kwa kuachana na tabia aliyoifanya.

Mkewe Suarez aitwaye Sofia amemtaka mumewe kubadili tabia ili kurudisha heshima yake kwa jamii inayoonekana kupotea.
Suarez ,26, amesimamishwa mechi kumi kutokana na kumuuma beki Branislav Ivanovic wa Chelsea.


Pamoja na kumuomba abadilike, mkewe amemsisitiza lazima ajifunze kujizuia kutokana na suala la hasira hasa zile za papo kwa hapo ambazo zimekuwa zikimuathiri.

Katika mahojiano na jarida la Liverpool, Suarez alisema: “Mke wangu ameniambia kuwa ninabishana sana na waamuzi na mabeki na inawezekana ndiyo maana ninakuwa na hasira kupita kiasi.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic