May 2, 2013



Kocha Mkuu wa Barcelona, Tito Vilanova amesema mshambuliaji wake, Lionel Messi hakuwa mgonjwa.

Vilanova amesema alilazimika kumuacha nje Messi baada ya kusema alikuwa anajisikia vibaya, hivyo akaamini asingeweza kuisaidia timu.


Barcelona ilikumbana na kipigo cha aibu cha mabao 3-0 katika mechi ya pili ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hivyo kufanya iwe imeondolewa na Bayern Munich kwa jumla ya mabao 7-0 ambayo ni rekodi mpya.


Messi alionekana katika benchi wakati Barcelona ikipambana na Wajerumani hao ambao ndiyo walitawala mchezo utafikiri wako nyumbani.

Wengi walitarajia kumuona Messi akiingia ili kuokoa jahazi, lakini badala yake, Vilanova alianza kuwatoa wachezaji tegemeo kama Xavi na baadaye Iniesta ikiwa ni dalili ya kukubali hawana ujanja dhidi ya Bayern maarufu kama Bavarians.

Messi alionyesha yuko safi katika mechi dhidi ya Athletic Bilbao (Jumamosi), lakini katika dakika za mwisho tukiwa tayari kwenye uwanja wa San Mames akaanza kujisikia tofauti,” alisema Vilanova.

“Jana (juzi) alifanya mazoezi na timu na ilionekana angecheza lakini baadaye mambo yakabadilika pia, ndiyo maana nasema hakuwa majeruhi, lakini niliona kutokana na hali hiyo asingekuwa msaada kwa timu.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic