May 18, 2013





Kipigo cha mabao 2-1 ilichokipata Real Madrid kutoka kwa wapinzani wao wakubwa Atletico Madrid kimemfanya kocha Jose Mourinho kumaliza msimu bila hata kombe moja.

Mechi hiyo ya fainali ya Copa del Rey ilimalizika kwa Atletico kushinda kwa mabao 2-1 ikitokea nyuma baada ya Madrid kupata bao katika dakika ya 14.




Diego Costa ndiye alisawazisha kwa Atletico kabla ya beki Mbrazil, Miranda kufunga bao la pili katika 99 baada ya mechi kwenda katika dakika 30 za nyongeza.

Mechi hiyo ilijaa vituko huku mara kwa mara Real Madrid wakilalamika kuhusiana na uamuzi wa refa ambaye alionekana mara kadhaa kuacha faulo zilizotakiwa kuelekezwa Atletico Madrid.




Mwamuzi huyo alimtoa nje Mourinho kwa madai ya kuonyesha utovu wa nidhamu lakini akamtoa Ronaldo kwa kumchezea rafu makusudi mchezaji wa Atletico ingawa picha za video zilionyesha Ronaldo alianza kufanyiwa madhambi kwa kuchotwa mtama lakini mwamuzi akauchuna.

Hata hivyo, bado Madrid wanapaswa kujilaumu kwa kupoteza nafasi nyingi zikiwemo zile kupitia Ronaldo, Benzema na Ozil ambazo zingeweza kuwapatia mabao.

Madrid imemaliza msimu bila kuwa na kombe na Mourinho tayari amethibitisha kuondoka, taarifa zinaeleza anarejea Chelsea ya England ambayo mkononi ina kombe la Europa League.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic