May 17, 2013



Holiday Inn


Protea Oysterbay..


Kila kitu kimekuwa ni siri, kambi za Simba na Yanga sasa zimehamia jijini Dar es Salaam.

 KAMBI YA SIMBA:







Awali Yanga walitaka kwenda Bagamoyo, lakini imeonekana kesho watakuwa na safari kurejea jijini Dar es Salaam.

KAMBI YA YANGA:






Sasa Yanga waliokuwa wameweka kambi mjini Pemba wako Dar es Salaam katika hoteli tulivu ya Protea Osyterbay ambako wachezaji wamepumzika kusubiri mechi ya kesho dhidi ya Simba.

Lakini Simba nao, wamerudi Dar pia wakitokea Unguja na kuweka kambi katikati ya jiji katika hoteli ya Holiday Inn ambayo miaka miwili iliyopita, Yanga waliweka kambi hapo.

Hoteli hizo za kitalii ni nadra kwa Yanga au Simba kukaa, lakini safari hii inaonyesha kiasi gani kila upande umepania kushinda mechi hiyo, hivyo suala la gharama si ishu kubwa tena kwao.

Umbali kutoka Oysterbay iliko Protea na Upanga, katikati ya jiji ilipo Holiday Inn si mkubwa. Takribani mwendo wa dakika sita au saba kwa gari linalotembea taratibu.
Usiri umeendelea kuwa mkubwa sana kila timu ikionyesha haitaki kuonyesha iko wapi ingawa ni sehemu za kisasa ambazo wangependa wajulinake wako hapo.

Imekuwa kawaida inapokaribia mechi ya watani, mara nyingi hisia za hujuma hutangulia hata zinapokuwa hazipo, ili mradi uoga na tahadhari kubwa inachukua nafasi.

Inawezekana kabisa kutokana na maeneo zilipoweka kambi, timu hizo kesho zikapita njia moja kwenda Uwanja wa Taifa kwa ajili ya kipute chao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic