May 17, 2013




Kiungo mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa ameahidi kufunga bao moja katika mechi ya kesho dhidi ya Yanga.

Simba na Yanga zinakutana kesho kwenye Uwanja wa Taifa, Dar katika mechi inayotarajiwa kuwa ya kusisimua.

Lakini gumzo ni Ngassa ambaye amesaini mkataba wa miaka miwili na Yanga ambayo atakutana nayo hiyo kesho.


Msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga amewaambia waandishi wa habari leo kwamba, taarifa za Ngassa kasaini Yanga au la, hawezi kuzikanusha au kuthibitisha lakini mchezaji huyo ameahidi kufunga bao hiyo kesho.

“Ngassa ni kati ya wachezaji waliofanya vizuri katika mazoezi yetu kule Zanzibar, kwa kifupi taarifa hizo za Yanga wala hazijamchanganya ingawa siwezi kusema ndiyo au la kuwa amesaini.

 “Lakini yeye ameahidi kuwa atafunga bao moja kesho, ila suala la kumpanga au kutokumpanga linabaki kwa kocha Liewig,” alisema Kamwaga.

Gazeti maarufu la Michezo la Championi ndilo liliandika stori ya Ngassa kusaini Yanga kwa miaka miwili.

Maana yake, baada ya mechi ya keshokutwa, moja kwa moja atajiunga na timu yake mpya.

Tayari mmoja wa viongozi wa Yanga amethibitisha Ngassa kujiunga na Yanga na anatarajiwa kutambulishwa mara moja baada ya mechi hiyo ya kesho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic