May 17, 2013


Mafisango wa pili kulia waliosimama akiwa na kikosi cha Simba msimu uliopita..

Wachezaji na waamuzi katika mechi ya kesho kati ya Yanga na Simba, watasimama dakika moja kutoa heshima na kumkumbuka aliyekuwa kiungo wa Simba, Patrick Mutesa Mafisango.

Mafisango raia wa DR Congo alifariki dunia Mei 17, 2012 katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Veta Chang’ombe jijini Dar es Salaam.


Msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga amewaambia waandishi wa habari leo kuhusiana na dakika moja hiyo kwa lengo la kumkumbuka na kumpa heshima Mafisango.

Wachezaji wa Simba watavaa vitambaa vyeusi katika mikono yao ikiwa ni sehemu ya kumkumbuka kiungo huyo.

Wakati wa uhai wake, Mafisango ambaye aliichezea Azam FC pia, alikuwa kiungo tegemeo wa Simba ambaye alileta mabadiliko makubwa kiuchezaji.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic