May 17, 2013



Mechi ya watani wa jadi, Yanga na Simba itaonyeshwa moja kwa moja na Chaneli ya Super Sport 9.

Ofisa Mauzo wa DStv Tanzania, Furaha Samalu amesema mechi hiyo ya kesho kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam itaonekana katika nchi zaidi ya 30 barani Afrika.
 
Mabosi wa DStv Tanzania
“Kweli tutaonyesha mechi hiyo, kila kitu kimekwenda vizuri na tunachosubiri ni mchezo tu,” alisema Furaha.

Mechi kati ya Yanga na Simba ni moja ya zile zilizo kubwa zaidi barani Afrika.


Mashabiki wengi Watanzania wanaoishi nje ya Tanzania wamekuwa na hamu ya kuiona mechi hiyo moja kwa moja.

Tayari joto lake liko juu na mashabiki wamekuwa wakihaha jijini Dar es Salaam kutafuta tiketi kwa ajili ya mechi hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic