May 24, 2013

Kumekucha, inaonekana kuna vita kali kati ya Yanga na timu ya Tunisia kuhusiana na kumsainisha Haruna Niyonzima.

Kiungo huyo amekuwa akiusumbua uongozi wa Yanga kwa takribani wiki moja sasa wakitaka asaini, naye anapiga chenga.

Awali kulikuwa na taarifa kwamba Niyonzoma alitaka kusaini Simba, lakini baadaye kumekuwa na taarifa ameamua kuachana na Msimbazi.
Ushindani umebaki kati ya Yanga na timu ya Tunisia ambayo amekataa kuitaja,.

“Kweli kuna timu ya Tunisia inanitaka, imenipa ofa nzuri lakini ninachotakiwa ni kutulia kwanza.


“Kwa sasa bado ni mchezaji wa Yanga, hivyo ninapaswa kutulia kama binadamu na kujua nini nitakifanya,” alisema Niyonzima.

Lakini taarifa nyingine za jana, zilieleza mmoja wa ‘majembe’ ya usajili ya Yanga, Abdallah Bin Kleb alikuwa anafanya juhudi za kuhakikisha anampata Niyonzima asaini Yanga kabla ya kuondoka.

Kiungo huyo raia wa Rwanda amekuwa gumzo kwa misimu miwili sasa tokea atue Yanga akitokea APR ya kwao Rwanda.

Hali hiyo inatokana na kuonyesha uwezo mkubwa na kuwa msaada mkubwa katika kiungo cha Yanga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic