June 18, 2013




Kutua kwa Carlo Ancelotti katika klabu ya Real Madrid maana yake ule mfumo wa Kocha Jose Mourinho utakuwa umekufa.

Mourinho amekuwa akitumia mifumo mbalimbali ikiwemo ile inayolazimisha timu kujilinda sana na kushambuliajia kwa kushitukiza.


Karibu kila timu aliyefundisha Muitaliano huyo amekuwa akitumia mfumo we 4-3-3 ambao asili yake ni nchini Italia.

Mfano wakati akiwa AC Milan alipata mafanikio makubwa akitumia mfumo huo na kubeba makombe lakini baadaye akafanya hivyo baada ya kutua Chelsea ya England ambako pia alibeba ubingwa.

Pamoja na hivyo, msimu uliopita Ancelotti aliendelea kufanya vizuri akitumia 4-3-3 akiwa na PSG nchini Ufaransa pia katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Kutokana na mfumo wake maana yake kuna baadhi ya wachezaji waliokuwa hawapati namba Real Madrid watapata nafasi ya kucheza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic